Monday, August 6, 2012

PUNDA ANGEKUWA PROFESa

Baba: Mbona unafeli kila mtihani mwanangu?
Mtoto:Sababu sina akili
Baba:Sasa ngoja nikupige fimbo ili uwe an akili
Mtoto:Ingekuwa fimbo ndio humfanya mtu kuwa na akili basi punda angekuwa PROFESA

Monday, July 2, 2012

WABABE RESTAURANT

WABABE RESTAURANT.
Ndugu mteja tafadhali zingatia yafuatayo kwa usalama wako ukiwa eneo hili (hatuna msamaha)
1. Hakikisha unasafisha vyombo vyote na meza kabla hujaondoka.
2. Unapohitaji chakula hakikisha unahela iliyokamili (katika chenji). Hatuna muda wa kuzunguka/ kuhangaika kutafuta chenji kwa sababu yako.
3. kama ukiagiza chakula na ukaletewa ambacho sioulicho hitaji lazima ule na kama bei ipo juu utaongeza hela kama bei ipo chini haturudishi hela ni uzembe wako.
4. Unapoagiza chakula hakikisha hujavaa spika masikioni (ear/head phones) kwani ni
dalili ya dharau.
5. Marufuku kuacha/kubakisha chakula (lazima umalize)
6. Marufuku kuomba namba za wahudumu wetu wakike (usifikirie hata kujaribu)
Tunatanguliza tahadhari kabla ya ajali,jitahidi kuzingatia hayo hapo juu.
Wako,Afisa Bora Huduma Bora kwa Wateja (Nina mkanda mweusi wa Judo)
Kwa niaba ya
KERO INVESTMENT CO.

Sunday, July 1, 2012

POMBE NOOOOOMA...

Jamaa mlevi anaingia kwenye bus na
kuweka begi kwenye siti ya mbele,
akadoz. Mlevi mwingine akaja akatoa lile begi na kukaa pale,
akadoz pia. Wakwanza anaamka akidhani anafungua begi yake
kumbe ni zip ya mlevi mwngne, akaweka mkono ndani na kuuliza, nani ameweka ndizi na
machungwa kwenye begi langu?

SHAROBARO


Wanafunzi wa shule flani waliambiwa watengeneze
t.v kwa kutumia mabox!
Siku ya kuleta hizo t.v wanafunzi wote wakaleta
mabox yao,kasoro dogo mmoja sharobaro alieleta
karatasi kubwaaaa
...
Mwalimu akamuuliza "We vipi mbona umeleta
karatasi?"
Dogo akamjibu "Hii ni plasma flat screen".

Saturday, June 23, 2012

BIBI NA MADAI YAKE

    HAKIMU: Bibi, hebu ieleze mahakama kilichotokea.
BIBI: Nilikuwa nimelala nyumbani kwangu usiku wa manane,mlango unavunjwa na anaingia huyu kijana, aliyesimama pale.
HAKIMU: Endelea, Bibi.
BIBI: Si, akanivua nguo zote na kunipanda.
HAKIMU: Enhee!
BIBI: Akawa anakata kushoto, mimi kulia. Alidhani mimi siyawezi!
HAKIMU: Enhee!
BIBI: Kila akikata, na mimi najibu! akikata na mimi nimo,hadi raha
HAKIMU: Haaa!sasa tatizo lililokuleta hapa mahakamani ni nini?
BIBI: Atengeneze ule mlango aliouvunja!